MAANA YA FASIHI

Fasihi ni sanaa ya lugha. Fasihi hutumia lugha kutoa sanaa mbalimbali katika jamii.
Tanzu za Fasihi
Kuna tanzu mbili kuu za fasihi, na kila utanzu una vipera vyake: Fasihi Simulizi na Fasihi Andishi:
1.     Hadithi (Ngano) - hekaya, mighani, visasili n.k
2.     Nyimbo - za jandoni, za ndoa, za kazi n.k
3.     Maigizo - michezo ya kuigiza, ngomezi n.k
4.     Tungo Fupi - methali, vitendawili n.k
1.     Hadithi Fupi - hadithi isiyokuwa ndefu iliyochapishwa katika mkusanyiko wa hadithi nyingine
2.     Riwaya - hadithi ndefu iliyochapishwa katika kitabu chake pekee
3.     Tamthilia - mchezo wa kuigiza uliowekwa kwa maandishi
4.     Ushairi* - mashairi yaliyoandikwa
Tofauti kuu kati ya fasihi simulizi na fasihi andishi ni kwamba Fasihi Simulizi huwasilishwa kwa njia ya mdomo au matendo ilhali Fasihi Andishi huwasilishwa kwa njia ya maandishi.

Tanbihi:Ushairi ni kipera cha nyimbo lakini pia mashairi yanaweza kuwa chini ya Fasihi Andishi, ikiwa yamechapishwa.

Comments

Popular posts from this blog

TOFAUTI KATI YA FASIHI SIMULIZI NA ANDISHI

UMUHIMU WA FASIHI